• UFUGAJI WA BATA BUKINI WENYE TIJA: SEHEMU YA PILI

    BATA BUKINI: UFUGAJI WENYE TIJA
     
    KUTAGA
    Bata Bukini huanza kutaga baada ya miezi saba na hutaga mara tatu kwa mwaka. Isipokuwa, utagaji wa bata bukini weupe na wa rangi hutofautiana katika idadi ya mayai
    Bata Bukini weupe hutaga mayai sita tu lakini wale wa mchanganyiko wa rangi hutaga mayai kumi na mbili (mara mbili ya weupe)


    KUATAMIA
    Jinsi ilivyotofauti katika idadi ya utagaji wa mayai hivyo ndivyo uwezo wa kuatamia pia ulivyo. Bata Bukini weupe huatamia mayai 6 na wale wa rangi huatamia mayai 12
    Ndege hawa huatamia kwa siku 29, huangua vifaranga kwa siku 3 na mara nyingi hutotoa mayai yote, si rahisi mayai kubaki bila kutotolewa au kuharibika.

    NAMNA YA KUTUNZA VIFARANGA
    Mara tu vifaranga wanapoanguliwa, wachukue na kuwatenga na mama yao kisha waweke katika banda safi lisilopitisha baridi. Unaweza kuwawekea taa ya umeme kama una uwezo ili kuwatengenezea joto.
    Pia, waweza kuzungushia banda lao kitu kizito kama blanketi ili kuwakinga na baridi au upepo.

    BANDA
    Bata Bukini wanahitaji nafasi ya kutosha hivyo andaa banda kulingana na wingi wa bata unaotarajia kufuga.
    Hakikisha banda limesakafiwa au banda la udongo lisilotuamisha maji au unaweza kuweka mbao au mabanzi kisha unaweka maranda ili kuwakinga na baridi.

    MAJI
    Ni lazima bata wapatiwe maji ya kunywa kila siku na hakikisha banda halikosi maji wakati wote. Safisha chombo cha maji na kubadilisha maji kila siku.
    Ndege hawa wanahitaji maji ya kunywa ya kutosha kama ilivyo kwa kuku. Hakikisha maji yako kwenye chombo ambacho hayatamwagika , kwani kumwagika kunaweza kusababisha kuibuka kwa magonjwa. Bata Bukini hawapendi uchafu. Hivyo maji yawe mahali ambapo hayatachafuka.




    SOURCE: FREBU Poultry Farm

    1 comment: