• UFUGAJI WA BATA BUKINI WENYE TIJA: SEHEMU YA TATU

    BATA BUKINI: UFUGAJI WENYE TIJA
     
    MAGONJWA
    Ni mara chache sana bata bukini kushambuliwa na magonjwa kama watawekwa katika hali ya usafi. Magonjwa yanayoweza kuwasumbua ni mafua na wakati mwingine kuharisha




    TIBA ZA ASILI
    Unaweza kutibu bata bukini kwa njia za asili. Tumia mwarobaini, vitunguu (maji na saumu).


    Mwarobaini: unaweza kutumia dawa hii kutibu mafua kwa bata bukini wakubwa au vifaranga.
    Maandalizi
    Chukua kiasi kidogo cha mwarobaini kisha twanga vizuri kupata maji maji. Kamua maji ya mwarobaini, kisha changanya na maji uliyo andaa kuwanywesha vifaranga.

    Kitunguu Saumu na Kitunguu Maji:
    Dawa hii hutumika kukinga na kutibu bata bukini wanaoharisha.
    Maandalizi
    Unachukua kitunguu saumu au maji na kuondoa maganda ya nje kisha safisha na kukata vipande vidogovidogo na kuwawekea kama chakula.Unaweza kuwapatia kila siku hadi watakapopona.
    Majani: Bata Bukini chakula chao kikubwa ni majani. Majani yana vitamini A, hivyo hakikisha unawapatia ya kutosha. Wapatie majani jamii ya mikunde.




    SOURCE: FREBU Poultry Farm 

    No comments:

    Post a Comment